Ingia / Jisajili

EE BWANA FADHILI ZAKO NI ZA MILELE Zaburi 137

Mtunzi: Pascal Mussa Mwenyipanzi
> Mfahamu Zaidi Pascal Mussa Mwenyipanzi
> Tazama Nyimbo nyingine za Pascal Mussa Mwenyipanzi

Makundi Nyimbo: Zaburi

Umepakiwa na: Pascal Mussa

Umepakuliwa mara 742 | Umetazamwa mara 2,172

Download Nota Download Midi
Maneno ya wimbo
Kiitikio: Ee Bwana fadhili zao na za milele, usiziache kazi za mikono yako, usiziache kazi za mikono yako usiziache kazi za mikono yako. 1.Nitakushukuru kwa moyo wangu wote,mbele ya miungu nitakuimbia zaburi, na nitasujudu nikilikabili, hekalu lako takatifu. 2.Nitalishukuru jina lako Mwenyezi kwa zako fadhili pia uaminifu wako, kwa maana umekuza ahadi zako kuliko jina lako Bwana. 3.Ingawa Mwenyezi Mungu yuko mbinguni amwangalia mnyenyekevu kwa wema naye amjua mwenye kujivuna, timiza mambo yote Mungu. 4. Nilipokuita wewe ukaniitikia, ukanifariji nafsi ukanitia nguvu, fadhili zako Bwana ni za milele usisahau kazi zako.

Maoni - Toa Maoni

Hakuna maoni kwenye wimbo huu

Toa Maoni yako hapa