Maneno ya wimbo
                KIITIKIO 
Nikupe nini (Ee Mungu) cha kupendeza (Ee Bwana) uwezo wangu ni mdogo waujua vizuri pamoja nayo dhiki inayonisonga mimi (u)ipokee sadaka yangu iliyo duni. x 2
MASHAIRI
1. Amka ndugu  tupeleke  mazao ya mashamba yetu (tena) tukamtolee na fedha za mifuko yetu (sisi).
2. Sina  cha kukutolea  lakini ipokee nafsi (yangu) ninayakabidhi maisha yangu uniongoze (Bwana).
3. Maisha yangu  ni ya dhiki Bwana wayajua vizuri (tena)  udhaifu  na unyonge wangu unaujua (Bwana).
4. Ni kazi za mikono yetu  Ee Bwana tunakutolea (Bwana) japo ni kidogo tunakileta ukipokee (Bwana).
            
                                    
                Nyimbo nyingine za mtunzi huyu