Ingia / Jisajili

Sala Yangu Ipae Mbele Yako

Mtunzi: David B. Wasonga
> Mfahamu Zaidi David B. Wasonga
> Tazama Nyimbo nyingine za David B. Wasonga

Makundi Nyimbo: Sadaka / Matoleo

Umepakiwa na: David Wasonga

Umepakuliwa mara 8,403 | Umetazamwa mara 22,162

Download Nota Download Midi
Maneno ya wimbo

Kiitikio:

Sala yangu na ipae mbele yako Bwana (Ee Bwana) kama moshi wa ubani altareni (x 2). Na ipae, na ipae kama moshi wa ubani na kuinuliwa kwa mikono yangu, iwe kama sadaka ya jioni.

Mashairi:

1. Tunakusihi Ee Bwana uipokee sala yetu, ipae mbele yako kama moshi wa ubani, iwe kama sadaka ya mtumishi wako Abeli.

2. Hata matoleo yetu, kazi za mikono yetu, twayaleta mbele zako kwa unyenyekevu mkubwa, twakusihi Ee Bwana uyatakase, uyapokee kama shukrani yetu.

3. Vipaji hivi tunavyokutolea, vikupendeze, vikupendeze, vipae mbele zako kama moshi wa ubani, viwe kama sadaka ya jioni.


Maoni - Toa Maoni

Butungo Apr 01, 2017
Wimbo uko vema sana huu

Gift Feb 01, 2017
Nimeipenda sanaaaa yaniiii

Toa Maoni yako hapa