Ingia / Jisajili

Utukufu Kwa Mungu (Misa Ya Mashahidi Wa Uganda)

Mtunzi: Dr. Nicholas Azza
> Mfahamu Zaidi Dr. Nicholas Azza
> Tazama Nyimbo nyingine za Dr. Nicholas Azza

Makundi Nyimbo: Misa

Umepakiwa na: Nicholas Azza

Umepakuliwa mara 420 | Umetazamwa mara 1,061

Download Nota Download Midi
Maneno ya wimbo
UTUKUFU KWA MUNGU JUU (Misa Ya Mashahidi Wa Uganda) Kitikio Utukufu kwa Mungu, utukufu kwa Mungu juu mbinguni. Na amani (pote!) duniani (kweli!), kwa watu wenye mapenzi mema. Mashairi 1. Tunakusifu, tunakubariki, tunakuabudu, tunakutukuza. Tunakushukuru kwa ajili ya utukufu wako mkuu, Ee Bwana Mungu, Mfalme wa mbinguni, Mungu baba, Ee Mungu Baba mwenyezi’ 2. Ee Bwana Yesu Kristo, Mwana wa pekee, Mwanakondoo wa Mungu . Uondoaye dhambi za dunia , utuhurumie. Uondoaye dhambi za dunia , pokea ombi letu. 3. Ewe mwenye kuketi kuume kwa Baba, utuhurumie. Kwakuwa ndiwe uliye peke yako Mtakatifu, Ee Bwana Yesu, kwakuwa ndiwe uliye peke yako Mkuu, Yesu Kristo. 4. Pamoja na Roho Mtakatifu katika utukufu wa Mungu Baba mwenyezi, Amina, Amina.

Maoni - Toa Maoni

Hakuna maoni kwenye wimbo huu

Toa Maoni yako hapa