Ingia / Jisajili

Uturehemu Ee Bwana

Mtunzi: Ernest Magunus
> Mfahamu Zaidi Ernest Magunus
> Tazama Nyimbo nyingine za Ernest Magunus

Makundi Nyimbo: Kwaresma | Zaburi

Umepakiwa na: ERNEST MAGUNUS

Umepakuliwa mara 585 | Umetazamwa mara 2,083

Wimbo huu unaweza kutumika:
- Katikati Jumatano ya Majivu
- Katikati Dominika ya 1 ya Kwaresma Mwaka A

Download Nota Download Midi
Maneno ya wimbo

Kiitikio:

||: Uturehemu Ee Bwana, Uturehemu Ee Bwana Uturehemu Kwa kuwa tumetenda dhambi :||

1. Ee Mungu, unirehemu, sawasawa na fadhili zako. Kiasi cha wingi wa rehema zako, Uyafute makosa yangu.

2. Unioshe kabisa na uovu wangu, Unitakase dhambi zangu. Maana nimejua Mimi makosa yangu, Na dhambi yangu I mbele yangu daima.

3. Nimekutenda dhambi Wewe peke yako, Na kufanya maovu mbele za macho yako. Ee Mungu, uniumbie moyo safi, Uifanye upya roho iliyotulia ndani yangu.

4. Usinitenge na uso wako, Wala roho wako mtakatifu usiniondolee. Unirudishie furaha ya wokovu wako.

5. Unitegemeze kwa roho ya wepesi. Ee Bwana, uifumbue midomo yangu, Na kiywa changu kitazinena sifa zako.



Maoni - Toa Maoni

Hakuna maoni kwenye wimbo huu

Toa Maoni yako hapa