Ingia / Jisajili

MUNGU WANGU JE! HUNISIKII? 2

Mtunzi: Wolford P. Pisa (WPP)
> Mfahamu Zaidi Wolford P. Pisa (WPP)
> Tazama Nyimbo nyingine za Wolford P. Pisa (WPP)

Makundi Nyimbo: Mafundisho / Tafakari

Umepakiwa na: Wolford Peter Pisa

Umepakuliwa mara 222 | Umetazamwa mara 1,487

Download Nota Download Midi
Maneno ya wimbo

KIITIKIO

Ee Bwana Mungu wangu je hunisikii, au ninaomba vibaya? au nina dhambi nyingi kuliko wengine (Bwana) 

zinazosababisha usinijibu.

MASHAIRI

  1. Maana nimekuomba, nimekuomba kwa muda mrefu, nimeona wengi walokuwa na matatizo kama yangu, ambao umeshawajibu Bwana, lakini mimi Bwana mbona sikuoni?
  2. Nimekusubiri kwa muda mrefu, sijakuona katika maisha yangu, hata nimekaribia nimekaribia  kukata tamaa, ndipo nikaamua kukuuliza, Ee Bwana, Bwana, Bwana Mbona sikuoni?
  3. Nilisubiri nikiamini, ya kwamba kwamba muda wangu bado, maana imeandikwa kila jambo na wakati wake, naamini sasa ni wakati wangu, Ee Mungu wangu nakuomba unijibu.

Maoni - Toa Maoni

Hakuna maoni kwenye wimbo huu

Toa Maoni yako hapa