Ingia / Jisajili

Mungu Wangu Mbona Umeniacha

Mtunzi: Dr. David S. Kacholi
> Mfahamu Zaidi Dr. David S. Kacholi
> Tazama Nyimbo nyingine za Dr. David S. Kacholi

Makundi Nyimbo: Juma Kuu | Kwaresma

Umepakiwa na: David Kacholi

Umepakuliwa mara 6,682 | Umetazamwa mara 15,865

Download Nota Download Midi
Maneno ya wimbo

Kiitikio: Mungu wangu Mungu wangu mbona umeniacha, Mungu wangu Mungu wangu mbona umeniacha x 2.

Mashairi:

1. Wote wanionao hunicheka sana, hunifyonya wakitikisa vichwa vichwa vyao.

2. Husema alimwamini Bwana naye amwokoe, amwopoe maana apendezwa naye.

3. Kwa maana mbwa wengi wamenizunguka, kundi la waovu wamenizingira.

4. Mikono na miguu wamenitoboa, naweza kuhesabu mifupa yangu yote.

5. Wanagawanya nguo wanagawanya nguo, wapigia kura kanzu kanzu yangu.

6. Bwana usisimame mbali mbali nami, ewe msa'da wangu uje hima kunisaidia.


Maoni - Toa Maoni

Victoria Michael May 07, 2017
Unanitia moyo ktk mapito yangu

Thomas pokella Apr 09, 2017
Mimi naomba wimbo huu mbali ya mashairi

Toa Maoni yako hapa