Ingia / Jisajili

Ni Neno Jema

Mtunzi: Alex Rwelamira
> Mfahamu Zaidi Alex Rwelamira
> Tazama Nyimbo nyingine za Alex Rwelamira

Makundi Nyimbo: Shukrani

Umepakiwa na: Alex Rwelamira

Umepakuliwa mara 9 | Umetazamwa mara 12

Download Nota Download Midi
Maneno ya wimbo

Ni neno jema kumshukuru kumshukuru Bwana na kuliimbia jina lako wewe uliye juu X2

Kuzitangaza rehema zako asubuhi na uaminifu wako wakati wa usiku

Kwa vifijo na vigelele kwa ngoma na furaha (mimi) nitaziimba sifa zako mbele za watu Ee Bwana jinsi lilivyo tukufu jina lako X2

1. Ee Bwana nitakutukuza siku zote za maisha yangu umeniumba mimi kwa jinsi ya ajabu daima sitaacha kiyasimulia matendo

2. Umenijalia mimi akili na utashi wa kuyajua mema na yale yaliyo mabaya Ee Mungu uliye mkuu sana kushinda vitu vyote

3. Nitakushukuru Mungu wangu kwa moyo wangu wote mbele ya miungu nitakuimbia zaburi nitasujudu nikilikabili hekalu lako Bwana


Maoni - Toa Maoni

Hakuna maoni kwenye wimbo huu

Toa Maoni yako hapa