Ingia / Jisajili

Sadaka Ya Shukrani

Mtunzi: F. K. Wambua
> Tazama Nyimbo nyingine za F. K. Wambua

Makundi Nyimbo: Sadaka / Matoleo

Umepakiwa na: francis wambua

Umepakuliwa mara 42 | Umetazamwa mara 89

Download Nota Download Midi
Maneno ya wimbo
IKUPENDEZE EE BWANA(F.K.WAMBUA Sop/Tenor: Nimeshika mikononi mwangu, zawadi ulonijalia, All: Ninakuja mbele zako Bwana, nitoe shukrani zangu Sop/tenor: Natembea kwa unyenyekevu, naileta sadaka yangu, All: Ninakuja mbele zako Bwana, nitoe shukrani zangu (Bass: nakuomba) ALL: Bwana uipokee, sadaka yangu ya leo, nayo ikupendeze kama ya Abeli)x2 1.S/A: Na fedha za mifuko ee Bwana (Upokee). Ingawa ni kidogo ee Bwana (Upokee). 2.S/A:Mkate na divai ee Bwana (Upokee). Ni jasho la wanao ee Bwana(Upokee). 3.S/A: Mazao ya mashamba ee Bwana(Upokee). Nafaka na mifugo ee Bwana(Upokee). 4.S/A: Nafsi zetu twaomba ee Bwana (Upokee). Furaha na uchungu ee Bwana (Upokee).

Maoni - Toa Maoni

Hakuna maoni kwenye wimbo huu

Toa Maoni yako hapa