Ingia / Jisajili

Chaguo Langu

Mtunzi: Thomas G. Mwakimata
> Tazama Nyimbo nyingine za Thomas G. Mwakimata

Makundi Nyimbo: Mafundisho / Tafakari | Ndoa | Shukrani

Umepakiwa na: Thomas George Mwakimata

Umepakuliwa mara 684 | Umetazamwa mara 1,671

Download Nota Download Midi
Maneno ya wimbo
1. Mpendwa wangu rafiki yangu ni fahari kuwa na wewe, Asante Mungu Mwenyezi kwa kumleta huyu nasema Wewe Ndiwe Chaguo langu Furaha ya Moyo Wangu, Faraja ya Nafsi yangu leo umekuwa wangu x 2. 2. Umeumbwa kwa ajili yangu ninaambatana na wewe, daima ni ubavu wangu nimeapa tena ni hakika (Kiitikio) 3. Njoo kwangu karibu yangu nakupenda mume wangu, unipende mimi ni wako siku zote uwe name kwani (Kiitikio) 4. Mwenyezi amenipa wewe mwanamke mwenye tunu bora wa thamani tena ni mzuri naahidi kwako ni kwakuwa (Kiitikio) KIBWAGIZO. I. Umebarikiwa Rehema leo umepata mume mwema umtunze umuheshimu, II. Joseph huyu ni wako ni mifupa na nyama yako siku zote ukampende, III. Kwa Sakramenti ya ndoa sasa nyinyi ni mwili mmoja mpendane siku zote, IV. Ni Agano hili Takatifu limewaleta nyinyi pamoja mshikamane kwa imani. HITIMISHO. ? Leo mume (Kweli) idhinishwa (Tena )mbele ya Altare ya Mungu, ? Ni Agizo (Hilo) lake Kristo ( Hivyo ) shikamaneni kwa upendo, ? Siku zote (Nyinyi) mpendane (Sana) kama leo mlivyoahidi, ? Nasi sote (kweli) tunasema (Tena) Mungu Mwenyezi awe nanyi.

Maoni - Toa Maoni

Hakuna maoni kwenye wimbo huu

Toa Maoni yako hapa