Ingia / Jisajili

Nisamehe Bwana

Maneno ya wimbo
NISAMEHE BWANA 1.Nisamehe Bwana mimi mtumishi wako, naja mbele yako naja na sala yangu, ninanyenyekea chini ya miguu yako, unitakase kwa makosa yangu yote Nimekosa kwa mawazo kwa maneno na kwa vitendo Bwana unihurumie Bwana mimi mwenye dhambi kwani nimekosa kutimiza wajibu wangu kama mkristu mimi unihurumie Bwana mimi mkosefu. 2.Sistahili mimi kuikaribia meza, wala hata kunena jambo lolote, nimejuta sana naomba huruma yako, unipokee mimi mtumishi wako 3.Ninapokuomba Bwana unisikilize, mahangaiko ya dunia mengi sana, yamenisonga kushoto hata kulia, mbele mbele na nyuma mimi sioni kitu 4.Ndugu zangu nao wananichekelea, ninapopambana na hali hali zangu, hivyo tumaini langu naliweka kwako, njoo hima Bwana wangu uniokoe

Maoni - Toa Maoni

Hakuna maoni kwenye wimbo huu

Toa Maoni yako hapa