Ingia / Jisajili

Nitakushukuru

Mtunzi: Dr. Basil B. Tumaini
> Mfahamu Zaidi Dr. Basil B. Tumaini
> Tazama Nyimbo nyingine za Dr. Basil B. Tumaini

Makundi Nyimbo: Shukrani | Zaburi

Umepakiwa na: Basil Tumaini

Umepakuliwa mara 2,756 | Umetazamwa mara 6,704

Download Nota Download Midi
Maneno ya wimbo

NITAKUSHUKURU

Mtunzi: Dr. Basil Tumaini

Wimbo wa Shukurani na sifa (taz. Zab. 138)

Kiitikio:

Nitakushukuru Bwana kwa neema zako

Mbele ya miungu nitakuimbia zaburi.

Nitakuimbia nyimbo za kukushukuru,

Kwa sauti tamu nitaimba sifa zako,

Kwa kinanda pia ngoma nayo matoazi,

Nitazitangaza sifa zako Mungu wangu.

Nitayatangaza matendo yako makuu,

Na fadhili zako nitaziimba milele.

Mashairi:

1.    Siku ile niliyokuita uliniitikia, ukanifariji nafsi yangu kwa kunitia nguvu.

2.    Wafalme wote wa dunia watakushukuru, watakapo yasikia maneno ya kinywa chako.

3.    Ingawa Bwana yuko juu amuona mnyenyekevu, naye amjua mwenye kujivuna tokea mbali.

4.    Nijapokwenda kati ya shida utanihuisha, na mkono wako wa kuume utaniokoa.

5.    Bwana atanitimilizia mambo yangu, maana fadhili zake Bwana ni za milele.


Maoni - Toa Maoni

Hakuna maoni kwenye wimbo huu

Toa Maoni yako hapa