Ingia / Jisajili

Njoni Nanyi Mtaona

Mtunzi: Dr. Basil B. Tumaini
> Mfahamu Zaidi Dr. Basil B. Tumaini
> Tazama Nyimbo nyingine za Dr. Basil B. Tumaini

Makundi Nyimbo: Miito

Umepakiwa na: Basil Tumaini

Umepakuliwa mara 749 | Umetazamwa mara 2,980

Download Nota Download Midi
Maneno ya wimbo

NJONI NANYI MTAONA

(Yn. 1:38-39)

Wimbo wa Wito

Mtunzi: Dr. Basil B. Tumaini (+255 767 847 258)

KIITIKIO

Yesu alipogeuka akawaona wakimfuata. Naye akawaambia, “mnatafuta nini?”

Wakamwambia,

“Rabi (Mwalimu), x 2

Wewe unakaa wapi?”

Naye Yesu akawaambia,

“Njoni, nanyi mtaona.”

Wakaenda wakaona akaapo, nao wakakaa kwake siku ile. X 2

VIIMBIZI

1.    (Mt. 10:16) Ninawatuma kama kondoo kati ya mbwa mwitu. Iweni werevu kama nyoka, iweni wapole kama njiwa.

2.    (Mt. 10:7) Mkahubiri: “Ufalme wa Mungu Umekaribia”. Fukuzeni pepo, poozeni magonjwa, wahubirini habari njema.

3.    (Lk. 10:20) Msifurahi kwa kuwa pepo wanawatii, bali kwa kuwa majina yenu yameandikwa Mbinguni.

4.    (Taz. Yn. 13:37 na Yn. 6:67-68) Tuwe tayari kuutoa uhai kwa ajili ya Kristo/

“Twende kwa nani, Wewe unayo maneno ya Uzima wa Milele.”


Maoni - Toa Maoni

Hakuna maoni kwenye wimbo huu

Toa Maoni yako hapa