Ingia / Jisajili

Nitakushukuru Kwa Moyo Wangu Wote

Mtunzi: David B. Wasonga
> Mfahamu Zaidi David B. Wasonga
> Tazama Nyimbo nyingine za David B. Wasonga

Makundi Nyimbo: Shukrani | Zaburi

Umepakiwa na: David Wasonga

Umepakuliwa mara 5,960 | Umetazamwa mara 13,648

Download Nota Download Midi
Maneno ya wimbo

Kiitikio:

Nitakushukuru kwa moyo wangu wote, nitakushukuru kwa moyo wangu wote, mbele ya Miungu nitakuimbia zaburi. Nitasujudu nikilikabili hekalu lako takatifu, nitalishukuru jina lako kwa ajili ya fadhili zako, kwa ajili ya fadhili zako na uaminifu wako.

Mashairi:

1. Nilipokulilia Ee Mungu, ulinijibu, wewe bwana ulinijibu, ulinijibu nilipokulilia.

2. Wafalme wa dunia watakusifu kwakuwa wamesikia maneno yako.

3. Ndipo wataimba sifa za matendo yako kwa maana utukufu wako ni mkuu, mkuu sana.

4. Ee Mungu, Ee Mungu utatimiza yote uliyoahidi, fadhili, fadhili, fadhili zako zikae nasi daima.


Maoni - Toa Maoni

daniel john Aug 23, 2017
Pongeza,

Edwin Ouma Aug 19, 2017
Wimbo huu umenibariki sana. Pongezi sana kwa watunzi wote. Mungu azidi kuwapa neema na afya ya kutunga nyimbo za kumtukuza. Baraka tele

wilson Apr 13, 2017
kazi nzuri mnayoifanya mbalikiwe!!!

Toa Maoni yako hapa