Chorus: Tupeleke vipaji vyetu kwa Mungu wetu Atabariki vipaji
	               Tukusanye mazao yetu twende tupeleke 
	               (eeeh ametujalia uhai na nguvu, nasi yatupasa twende tupeleke)x2
	1a) Vipaji hivi Baba twakutolea, kazi ya mikono yetu uvibariki
	   b) Mkate huu Baba pia divai, tunakutolea Baba uvipokee.
	2a) Na fedha hizi Baba twakutolea, japo ni kidogo Baba uzipokee
	   b) Mazao yetu Baba twakutolea, kazi ya mikono yetu uibariki
	3a) Furaha yetu Baba twakutolea, na udhaifu wa mwili utubariki
	   b) Matendo yetu Baba twakutolea, pia na mawazo Baba utubariki
	4a) Juhudi zetu Baba bidii yetu, tunazikabidhi kwako uzibariki
	   b) Uchungu wetu Baba na shida zetu, tunajikabidhi kwako utubariki
	5a) Watoto wetu Baba wazazi wetu, tunakutolea Baba uwabariki
	   b) Mashamba yetu Baba mifugo yetu, vyote mali yakoBaba uvibariki.