Ingia / Jisajili

Bwana Yesu Tunakuabudu

Mtunzi: Alfred Ogombo
> Mfahamu Zaidi Alfred Ogombo
> Tazama Nyimbo nyingine za Alfred Ogombo

Makundi Nyimbo: Ekaristi / Komunio

Umepakiwa na: Alfred Ogombo

Umepakuliwa mara 494 | Umetazamwa mara 2,322

Download Nota Download Midi
Maneno ya wimbo

Bwana Yesu tunakuabudu tunakiri U katika Hostya

Vichwa vyetu tunaviinamisha, na magoti tunakupigia

Maumbo ya mkate na divai, umo ndani tunakuabudu

1.Mwili wako  ni chakula kweli, damu yako ni kinywaji kweli –

   Twasadiki U katika Hostya, umo ndani kweli twasadiki

2.Umetupa chakula cha mbingu, tukiula hatuoni njaa

   Umetupa kinywaji cha mbingu, tukiinywa hatupati kiu

3.Maji ya ubavu wako Bwana, yatutakasa daima sisi –

   Kweli tunapata msamaha, kwa makosa tunayoyatenda

4.Umo humo Bwana wetu Yesu, twakuabudu twakusujudu –

   Tunaamini umungu wako, wajitokeza kwenye altare


Maoni - Toa Maoni

Hakuna maoni kwenye wimbo huu

Toa Maoni yako hapa