Maneno ya wimbo
                KWA BWANA KUMEKAMILIKA 
1. Neno moja nimemwomba x2 Mungu Mwenyezi 
Nalo ndilo nalisaka x2 Daima milele 
Nikae nyumbani mwake siku zote, nipate faraja maishani mwangu { (kwani) 
baraka zake (ni) nyingi, uzima wake (ni) mwingi na neema zake ni yeye ametupa } x2
( Nikae nyumbani mwake siku zote nipate faraja maishani mwangu ) x2
2. Mimi ninakaza mwendo x2 Nisichelewe 
Niende nikamwone Yesu x2 Nimshukuru 
3. Njoni kwangu ninyi nyote x2 Na mizigo yenu 
Mimi nitawapumzisha x2 Mkaishi huru 
4. Shambani mwake ee Bwana x2 Mavuno ni mengi 
Hivyo nitakwenda mimi x2 Nikayavune yote
            
                                    
                Nyimbo nyingine za mtunzi huyu