Maneno ya wimbo
                MUNGU NI YULE  YULE
MWANZO
Mungu ni yule -Mungu ni yule, jana na leo - na milele,  Mungu ni yule- Mungu ni yule, (Mungu ni yule yule yule) x2 
Ndiye yeye Mungu mmoja (Mungu yeye ndiye) aliyekuwa ndiye yeye Mungu mmoja aliyeko, ndiye yeye Mungu mmoja (Mungu yeye ndiye) ‘takaye kuwa ndiye yeye Mungu wa kweli anaishi, ndiye yeye Mungu mmoja (Mungu yeye ndiye)  wa baba zetu ndiye yeye yule Mungu, wa milele, 
Ni Mungu wa jana ni Mungu wa milele, Mungu wetu habadiliki  (Mungu) ni yule yule jana leo na milele (Mungu) ni  (ni Mungu ni) yule yule, kiangazi hata masika (Mungu) ni yule yule jana leo na milele (Mungu) ni  (ni Mungu ni) yule yule,
 Yeye ndiye alfa na omega mwanzo na pia mwisho hakuna mwingine kama yeye, (ni yeye ndiye) Bwana wa mabwana Mfalme wa wafalme hakuma mwingine kama yeye
1.Viumbe ulivyoumba vinakutuza kwa furaha vinasifu jina lako baba, na vile hatuvioni  pia vya kusifu, kwa maana wewe Mungu haubadiliki
2.Ukaumba ulimwe-ngu kwa ne-no lako, nchi kavu na bahari ukavitawanya, usiku ukawa giza mchana mwangaza,  sifa zako zinadumu kwa vizazi vyote 
MWISHO
Mungu aliyekuwa tangu mwanzo wa dunia na Mungu aliyeko sasa 	Mungu ni yule yule
Mungu aliyeumba ulimwengu kwa masiku na Mungu aliyeko sasa  	Mungu ni yule yule 
Alliyeikomboa israeli toka misri na Mungu aliyeko sasa ni		Mungu ni yule yule 
(ni yeye Mungu tangu mwanzo na Mungu ‘ko sasa)			ni yule yule    
Habadiliki kamwe -Mungu ni yule yule
Daima na milele -Mungu ni yule yule
Aliyetukomboa -Mungu ni yule yule 
Na ndiye yuko sasa - Mungu ni yule yule 
Basi na tumwimbie -Mungu wetu nyimbo za ushindi 
Tumchezee kwa furaha Mungu tumsifu 
He na sauti tuzipaze sauti za shangwe 
Tumwimbie Mungu wetu nyimbo za ushindi 
Ho na vifijo tuvipige tumfanyie shangwe  
Tumwimbie Mungu wetu nyimbo za ushindi
(tumpigie makofi tena makofi kwake muumba makofi Mungu atupenda ) x3 Mungu ni yule yule.
            
                                    
                Nyimbo nyingine za mtunzi huyu