Ingia / Jisajili

Nipisheni Nikahubiri

Mtunzi: Elijah M Kilonzi
> Mfahamu Zaidi Elijah M Kilonzi
> Tazama Nyimbo nyingine za Elijah M Kilonzi

Makundi Nyimbo: Mafundisho / Tafakari

Umepakiwa na: ELIJAH Mulei

Umepakuliwa mara 547 | Umetazamwa mara 1,415

Download Nota Download Midi
Maneno ya wimbo
1. Hebu nipisheni wote, nawasihi nipisheni x2 {Nihubiri neno njema, duniani kwa kuimba Kwani kuimba ni sawa, na kusali mara mbili} x2 Hebu nipishe shetani; nikahubiri x2 Hasira nyingi unaleta-kusudi nisihubiri Ubishi pia “ “ “ Udaku pia “ “ “ Vikwazo vingi “ “ “ Lakini nitahubiri. 2. Roho mtakatifu shuka, niongoze nikiimba x2 {Niguse roho za wale, wasiomwamini Yesu Kusudi wajiunge, na kundi la kondoo wake} x2 3. Baba, mama hata ndugu , nawasihi nipisheni x2 {Nijulishe watu Yesu ndie njia, kweli, uzima Wakifuata Bwana Yesu wataenda hadi mbinguni} x2 4. Bibi na watoto wangu, nawasihi nipisheni x2 {Niimbe niburudishe wanaopenda mziki Hivyo basi kwa kuimba nivute wengi kwa Bwana} x2 5. Jamii na marafiki, nawasihi nipisheni x2 {Niimbe niwafariji wenye shida mbalimbali Pia niwakumbusheni Bwana huyaweza yote} x2 6. Ee Bwana uwaongoze waimbaji duniani x2 {Kuimba kwao kuweze kueneza neno lako, Kufariji, hata pia kuweze kuburudisha} x2

Maoni - Toa Maoni

Hakuna maoni kwenye wimbo huu

Toa Maoni yako hapa