Ingia / Jisajili

Bwana Alitutendea Mambo Makuu

Mtunzi: James Muola Vavu
> Mfahamu Zaidi James Muola Vavu
> Tazama Nyimbo nyingine za James Muola Vavu

Makundi Nyimbo: Zaburi

Umepakiwa na: James Vavu

Umepakuliwa mara 159 | Umetazamwa mara 669

Download Nota Download Midi
Maneno ya wimbo
Bwana alitutendea mambo makuu; Bwana alitutendea mambo makuu; Tulikuwa tukifurahi, tulikuwa tukifurahi! x 2 1. Bwana alipowarudisha mateka wa Sioni, Tulikuwa kama wanaoota ndoto. Hapo kinywa chetu, kilijaa kicheko, Na ulimi wetu, kelele za furaha. 2. Ndipo waliposema kati ya mataifa, “Bwana amewatendea makuu.” Bwana alitutendea mambo makuu, Tulikuwa, tulikuwa tukifurahi! 3. Ee Bwana, uwarudishe wafungwa wetu, Kama vijito huko Negebu. Waliopanda kwa machozi watavuna Kwa kelele, kelele za furaha. 4. Anayekwenda huku akilia,akichukua Mbegu za kupanda, mbegu za kupanda. Atarudi kwa kelele, kelele za furaha, Akibeba, akibeba miganda yake.

Maoni - Toa Maoni

Hakuna maoni kwenye wimbo huu

Toa Maoni yako hapa