Ingia / Jisajili

Bwana Ametualika

Mtunzi: Alfred Ogombo
> Mfahamu Zaidi Alfred Ogombo
> Tazama Nyimbo nyingine za Alfred Ogombo

Makundi Nyimbo: Ekaristi / Komunio

Umepakiwa na: Alfred Ogombo

Umepakuliwa mara 1,076 | Umetazamwa mara 2,980

Download Nota Download Midi
Maneno ya wimbo

1.Bwana ametualika kwa karamu takatifu,

   tujongee ametuandalia chakula

   Kimeandaliwa leo kwa ajili yetu sisi,

   wanadamu tule tujaliwe wokovu

Tule mwili wake Bwana ni chakula cha uzima twende ndugu twende

Tunywe damu yake Bwana ni kinywaji cha uzima twende ndugu twende

2.Nasi tumetunukiwa tuzo hilo la milele,

   heri yetu tumeandaliwa karamu

   Neema tunazipata roho zetu zinaponywa,

   tunaimarika katika nyoyo zetu

3.Cheo zetu na mamlaka heshima tunayopewa,

   mbele zake Mungu sisi sote ni sawa

   Hivyo yatupasa sote tunyenyekee mbele zake,

   ndiye ametujalia haya maisha

4.Heri yetu heri yetu tuliyoitika wito,

   wa kushiriki kwenye karamu ya Bwana

   Tuepukane na dhambi tutende yaliyo mema,

   hapo ndipo tutamfurahisha Mwenyezi


Maoni - Toa Maoni

Hakuna maoni kwenye wimbo huu

Toa Maoni yako hapa