Ingia / Jisajili

Katika Vyombo Vya Udongo

Mtunzi: Br. Stan Mkombo, Ofmcap
> Tazama Nyimbo nyingine za Br. Stan Mkombo, Ofmcap

Makundi Nyimbo: Mafundisho / Tafakari | Miito | Shukrani

Umepakiwa na: Stanslaus Mkombo

Umepakuliwa mara 612 | Umetazamwa mara 2,447

Download Nota Download Midi
Maneno ya wimbo

KATIKA VYOMBO VYA UDONGO  [Br. Stan  Mkombo, OFMCap.]

1. Tumebeba hazina takatifu ya Mungu katika vyombo vya udongo; vyombo ni nafsi zetu zilizo dhaifu x2

Chorus

Sifa, utukufu milele viwe kwa Mungu Baba, na kwa Mwana, na Roho Mtakatifu.

Ndiye aliyetuwezesha kufika hata hapa; asifiwe, ahimidiwe milele.

2. Ili idhihirike wazi kuwa uwezo unaotenda kazi yake ndani mwetu si wetu, bali ni wa Mungu. x2

3. Tunasema asante Mama Maria, Fransisko na Watakatifu wote, nanyi wapendwa kwa sala na misaada. x2

[Baada ya Chorus ya mwisho malizia kwa kuimba Coda maneno yafuatayo]

Asante Baba, asante Mwana, Asante Roho Mtakatifu. x2


Maoni - Toa Maoni

Hakuna maoni kwenye wimbo huu

Toa Maoni yako hapa