Ingia / Jisajili

Ninayo Furaha

Mtunzi: Alfred Ogombo
> Mfahamu Zaidi Alfred Ogombo
> Tazama Nyimbo nyingine za Alfred Ogombo

Makundi Nyimbo: Mafundisho / Tafakari | Shukrani

Umepakiwa na: Alfred Ogombo

Umepakuliwa mara 510 | Umetazamwa mara 2,406

Download Nota Download Midi
Maneno ya wimbo

1.Ninayo furaha, ninapomwimbia Yeye Bwana Mungu wangu

   Nitamsifu Bwana nitamtukuza Bwana

   Bwana kaniepusha nayo majanga 'kanipa afya njema

   Nitamsifu Bwana nitamtukuza Bwana

  Daima nitamtumikia Mungu nitaimba milele utukufu wa Bwana sifaze ntatukuza x2

2.Bwana kanilinda, Bwana siku zote hunitendea makuu –

   Hivyo sinabudi mimi kumshukuru Mfalme Bwana Mtawala –

3.Sote tutambue, Bwana ni mkuu hakuna Mungu kama Yeye –

   Mbinguni duniani hakuna anayelinganishwa na Mungu –

4.Bwana astahili, kusifiwa na kutukuzwa milele yote –

   Jina lake takatifu na tukufu nalo lihimidiwe –

5.Bwana wa mabwana, Mungu wa miungu ndizo sifa zake Bwana –

   Mungu wa Ibrahimu Mungu wa Isaka Mungu wa Yakobo –


Maoni - Toa Maoni

Hakuna maoni kwenye wimbo huu

Toa Maoni yako hapa