Ingia / Jisajili

Twakutolea Sadaka Yetu

Mtunzi: Alfred Ogombo
> Mfahamu Zaidi Alfred Ogombo
> Tazama Nyimbo nyingine za Alfred Ogombo

Makundi Nyimbo: Sadaka / Matoleo

Umepakiwa na: Alfred Ogombo

Umepakuliwa mara 1,948 | Umetazamwa mara 4,575

Download Nota Download Midi
Maneno ya wimbo

Twakutolea sadaka yetu moja (wapo) ya vitu vingi ambavyo umetujalia kwa neema yako Bwana (na sasa) Twanyenyekea Bwana Mungu Mkuu uzipokee na uzibariki

 1.Sadaka yetu, na ikupendeze, iwe shukrani

   (yetu) kwa yale mema yote tupatayo kwako

2.Twakusihi, Mungu tuepushe, mabaya yote

   (Wewe) tumaini letu na upokee na shida zetu

3.Sifa zote, ee Bwana pokea, hapa tulipo

   (ume)-tufikisha kwa uwezo wako ulio mkuu

4.Mimi kiumbe, chako dhaifu, mwanga wako na

   (uni)-ongoze na unipokee jinsi nilivyo Bwana

5.Maombi yangu, na yakufikie, nakutolea

   (kwa we)-ma wako Mungu yatakase na uyabariki

6.N’ni cha thamani, nikupe Mungu? Sina mi’ ila

   (kido)-go ninacho kwa moyo wangu wote nakutolea


Maoni - Toa Maoni

Hakuna maoni kwenye wimbo huu

Toa Maoni yako hapa