Ingia / Jisajili

Tumrudishie Bwana

Mtunzi: Cpa M. B. Ngooh
> Mfahamu Zaidi Cpa M. B. Ngooh
> Tazama Nyimbo nyingine za Cpa M. B. Ngooh

Makundi Nyimbo: Sadaka / Matoleo

Umepakiwa na: Melkior Ngooh

Umepakuliwa mara 306 | Umetazamwa mara 1,421

Download Nota Download Midi
Maneno ya wimbo

Kiitikio:

Tuamke sasa (twendeni kwa Bwana) tukamtolee dhabihu, dhabihu za kumshukuru, tumrudishie (Bwana) kwani vyote tulivyo navyo ni mali yake, (kumtolea Mungu) ni kutengeneza njia ya wokovu, wokovu wa Milele X2

Mashairi:

  1. Tutoe kwa moyo, asema Bwana, nikitoa mali zangu zote kuwalisha maskini, kama sina upendo mimi, haisaidii kitu.

  2. Tutoe bila manung’uniko, asema Bwana, nikitoa mwili wangu wote, mwili wangu niungue moto, kama sina upendo mimi, haisaidii kitu.

  3. Ikiwa una neno na ndugu yako, kapatane nae ndipo urudi utoe sadaka yako, hapo ndipo sadaka yako itampendeza Mungu. 


Maoni - Toa Maoni

Hakuna maoni kwenye wimbo huu

Toa Maoni yako hapa